Featured Posts

Friday, August 29, 2014

TATIZO LA UKE MLEGEVU...JE UKUBWA AU UZURI WA UKE NI KITU CHA MUHIMU

Je ukubwa au uzuri wa uke ni kitu cha muhimu? Kama tunazungumzia mtu mwenye njaa, hapa kiasi kidogo cha chakula kitaweza kumshibisha, na kama chakula hicho hakikupikwa vizuri, pia mtu mwenye njaa atahangaika sana.
Mambo ya njaa na uke wa mwanamke vinahusiana vipi? Mtu anaweza kuuliza, jibu ni "KUTOSHEKA". Kama mtu ataweza kutosheka kutokana na chakula alichokula, jambo hilo linaleta amani. Ukubwa wa uke unaweza kuchangia sana kwa mwanaume kukosa raha ya tendo la ndoa. Iwapo unajua kuwa tatizo liko kwako na sio kwamba mumeo ana uume mdogo, hapo ni muhimu kwako utafute njia ya kupungua ukubwa wa uke wako.
Je kuna njia ya kugundua kama una uke mkubwa au mdogo?
Wanawake wengi hawajui ukubwa wa uke wao kwa kuwa hawawezi kujipima au kuona umuhimu wa kufanya hivyo. Uke unapokuwa katika hali yake ya kawaida kuta zake zinalaliana na kwa wengi kipenyo cha uke hakizidi inchi 1 hadi 1 na nusu na urefu wake kati ya inchi 3 hadi 4. Hata hivyo ukubwa wake hubadilika mwanamke anapokuwa tayari kwa tendo la ndoa. Unaweza ukadhani kuwa inchi 1 au 1 na nusu ni ndogo kwa mwanaume kupitisha uume wake, ukweli ni kwamba uke una uwezo wa kutanuka ili uweze kumeza uume. Ukiingia ndani ya uke,ukubwa huongezeka zaidi hadi kufika inchi 3.
Kwa wanawake waliozaa hawana budi kukubalina na ongezeko la ukubwa wa uke wao, kadri watoto wanvyoongezeka ndivyo ukubwa wa uongezekavyo. Hali hii hutokana na uharibifu wa misuli iliomo katika kuta za uke.

TUMEAMIA HUKU