Featured Posts

Monday, June 9, 2014

SIMULIZI NA KISA CHA KWELI, "KUPENDA KULINIPONZA " IFATILIA UPATE UHONDO HAPA


Ndani ya gereza la segerea Robert anamsimulia rafiki yake Richie ambae ni mwandishi wa habari kuhusu kesi yake ya mauhaji.
Ilikuwa mwaka jana mwezi wa kumi na mbili siku ya sikukuu ya x-mas .Nilikuwa na kipenzi change Queen chumbani ,nikamuuliza swali.Ujue nakupenda sana Quen?Hata mimi nakupenda Richie .Nitaamini vipi kama kweli unanipenda ?Sitokuacha mpaka fedha zako zitakapoisha.Ahaa , Queen ina maana unanipendea pesa?Ehee babu ,kwani ulikuwa ujui ?Mwanaume pesa ,suruali hata wanawake tunavaa.Ahaa Queen unasemaje ?Ehee ni mambo y a digital hayo tushaama analogy siku nyingi pesa kwanza mapenzi yanafuata.


Nilisikia kama mshale umeuchoma moyo wangu ,maumivu niliyoyapata sijui nisemeje.Nikabaki nimeduwaa huku nikishika moyo wangu na kujiuliza moyoni.Queen yule niliyekutana nae kijijini Lamadi Mwanza nilipokwenda kwenye harusi ya mjomba ,babu yake aliponiona akaniomba nimsaidie mjukuu wake kwenda Dar e salaam akatafute maisha kwani maisha ya kijijini ni magumu ,nikakubali.Aliponionyesha mjukuu wake hakika alikuwa ni mzuri ila uzuri wake ulifichwa na kumezwa na umaskini pamoja na maisha magumu ya kijijini pale nilimpenda palepale.Nikaongea na wazee Queen awe mchumba wangu wakakubali na nikakamilisha taratibu zote na kumchumbia Queen na kuondoka na Queen mjini .Cha kwanza ulipofika mjini nikampeleka saloon akapigwe soapsoap hakika alivutia kila mtu alimsifia .Nikamuanzisha masomo ya sekondari katika shule binafsi kwa maana muda huo alikuwa na miaka 16 na mimi miaka 26 tukawa tunaishi kama mke na mume ingawa ni kosa kisheria.Baada ya kumaliza kidato cha sita nikampeleka Havard university Marekani akasomee shahada ya kwanza ya utawala wa biashara.Ili kumuonyesha ni jinsi gani nampenda alipohitimu Havard nikampeleka Australia akasomee shahada ya pili ya utawala wa biashara.Alipohitimu na kurudi bongo nikamnunulia kampuni ya clearing and forwarding ahisimamie yeye,ikamnunulia na gari ,nikajenga nyumba mpya ya kisasa Tegeta,nikanunua na mashamba 3 pale Kibaha kwani nilijiona sasa natarajia kuwa baba wa familia na kuandika jina lake katika hatimiliki vya vitu vyote kumuonyesha ni jinsi gani ninavyompenda kwani nilijua ni mama wa watoto wangu mtarajiwa kwani mda si mrefu tungefunga ndoa .Looh Queen ananijibu hivi leo ?Rafiki yangu Samwel aliniambia Queen ana mwanaume mwingine ambae ni mkurugenzi wa fedha benki kuu ya Tanzania(BoT) kwani huwa anawaonaga New African Hotel mara kwa mara yeye akiwa anafuatiliaga malipo yake ya kupelekaga tenda ya magunia ya mchele hotelini hapo.Nikafanya uchunguzi kwenye simu ya Queen nikakuta ameweka password nikamvizia siku moja usiku amelala nikaichukua simu yake na kuna fundi simu niliwasiliana nae pindi nitakapoipata simu ya Queen basi aje haraka nyumbani kwangu aiondoe password , nikampigia aje .Fundi alipofika akaondoa password na nikayaona mawasiliano ya Queen na mkurugenzi wake na siku inayofuata walikuwa na miadi ya kukutana kule hotelini saa 9 alasiri, aisee moyo uliniuma sana baada ya hapo fundi alinishauri ili Queen asijue kama tumeondoa password katika simu yake basi tuipasue kwa kuindondosha chini na isiweze kuwaka tena ,nikafanya hivyo na kuipeleka chini ya kitanda sakafuni ikionekana imedondoka kutoka kitandani.Kesho yake ambayo ni sikukuu ya x-mas nikamshtua Samwel ili tukashuudie.Laa haula kweli walifika pale wakiwa wamekumbatiana wakipigana mabusu motomoto ,kushikana shikana kwa sana ,denda nje nje .Mimi na Samwel tulikaa mwisho kabisa kwenye kona tukiona kila kitu kinachoendelea.Hasira na wivu zikapanda nikataka kuinuka nikawazuru Samwel akaniwahi na kiniambia tulia Robert mwanamke hapigwi dunia itampiga.Nilishindwa kuendelea kuvumilia kuwaangalia nikamwambia Samwel tuondoke tukapitia mlango mwingine wa nyuma na kurudi nyumbani nikiwa na hasira kuu na mawazo mengi .
Na mda hule ananijibu vile alikuwa amerudi kutoka kule hotelini akiwa amelewa nikazidi kushangaa Quen huyu huyu siku hizi ni mlevi wa pombe dah inauma sana.Nikamuuliza nikiishiwa pesa itakuaje ?Maihii jibu alilonipa “Nakuacha ,kwanza mimi ni mwanamke mzuri na mrembo bwana ,pili ni msomi na kila mwanaume ananitaka maskini kwa matajiri ila mimi ninaangalia pesa kwanza”.Aha ,nilijikuta nipo jikoni nikachukua kisu ,nikaenda stoo nikachukua panga na shoka .Niliporudi chumbani nikamkuta amelala kifudifudi ,nikainua shoka kwa nguzu zangu zote ikatua kwenye shingo yake, kichwa kule kiwiliwili kule damu chapachapa .Nikachukua panga nikamkata mikono ,mapaja ,miguu na kuviweka vipande vipande.Nikayashika makalio yake anayolingia nikachukua kisu nikakata minofominofu ,nikaja kwenye maziwa yake yaliyosimama kama embe nyonyo nikayakata yote .Nikatoboa tumbo lake lililo flat na kutoa moyo ,mapafu,maini,bandama na nikatia vyote kwenye kiroba .Kichwa nikmpeleke mjumbe wetu nyumbani kwake usiku huo huo miguu nikampelekea mama wawili jirani yangu,mapaja nikampelekea baba Koku muuza chipsi pale mtaani kwetu.Utumbo ,minofu ya makalio,mapafu,moyo,maini ,bandama nikampelekea bi Kidawa mwanamke mmbeya mmbeya sana pale mtaani.Kila niliyempelekea alishangaa na damu imetapakaa kwenye nguo zangu wakapiga makelele jamani kaua mtu huyo.Watu wakatoka majumbani ,wakanikamata na kunipeleka kwa mjumbe ,mjumbe akaamuru nipelekwe polisi.Kichapo nilichopewa polisi nikapoteza fahamu na kuja kuzinduka nikajikuta nikiwa mahabusu keko.Uchunguzi ulipofanyika nikaonekana nimeua kwa kukusudia na siku ya hukumu nikaukumiwa kifungo cha maisha jela.Robert analia kupenda kumemponza.
MWISHO.

TUMEAMIA HUKU