Featured Posts

Sunday, June 29, 2014

Mwanamke Huyu Arejesha SHANGA Kanisani...JIONEE HAYA MAAJABU!!

Stori:MWANDISHI WETU, Arusha Katika hali ya kushangaza, mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina la Asnath Terevaeli hivi karibuni aliamua kukabidhi kanisani shanga za majini kwa kile alichodai kuwa, zimekuwa zikimtesa na kumfanya akose amani.
Mwanamke anayefahamika kwa jina la Asnath Terevaeli akikabidhi shanga kwa Mchungaji Kiongozi, (Frank Endrew) wa Kanisa la Ufufuo na Uzima mkoani Arusha. Tukio hilo lilijiri mwishoni mwa wiki iliyopita katika Kanisa la Ufufuo na Uzima mkoani hapa baada ya moto wa Injili kuwashwa na Mchungaji Kiongozi, Frank Endrew. Akizungumza na Risasi Jumamosi, mmoja wa waumini wanaosali kanisani hapo aliyejitambulisha kwa jina la Yusta John alisema, awali mwanamke huyo alionekana mwenye jambo linalomtatiza na lilipotolewa tangazo la wenye matatizo kupita mbele, Asnath alifanya hivyo huku akiwa ameshika shanga mkononi. “Watu wengi walikuwa na shauku ya kujua lililomsibu mama huyo lakini alipofika alimkabidhi mchungaji Frank shanga hizo zilizotengenezwa kiasili zinazodaiwa ni za majini. “Mwenyewe alieleza kuwa, alipewa kama zawadi na mwanaye lakini cha ajabu zimekuwa zikimtesa na kumfanya akose amani.
Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima. 

TUMEAMIA HUKU