Featured Posts

Friday, June 27, 2014

WOLPER KUKIONA CHA MOTO, NI KUHUSU TABIA YA KUHAMAHAMA DINI

Staa wa filamu za Kibongo, Jacqueline Wolper akipozi.
Wolper kiimani ni Mkristo lakini hivi karibuni alibadili na kuwa Muislam kabla ya kurejea tena kwenye imani yake ya awali ya ukristo.
Sababu ya Wolper kubadili dini ilikuwa ni kufunga ndoa na aliyekuwa mchumba wake Abdallah Mtoro ‘Dalas’, walipoachana akaamua kurudi kwenye ukristo.
Akizungumza na Risasi Jumamosi juzikati, Shehe Salum, alisema Wolper anapaswa kujichunguza na kubadilika haraka kwani kitendo anachofanya ni kinyume na taratibu za dini.
“Siyo vizuri hata kidogo na hata dini zote zinakemea kitendo cha kuchezeachezea dini kwani ni chukizo kwa Mungu.
Jacqueline Wolper akiwa kazini.
“Kwa upande wa Dini ya Kiislamu, kuna sheria kali zaidi kwa mtu akionekana na tabia hiyo, anaweza hata kuuawa hivyo wanaofanya mchezo huo waache kwani siyo vizuri. Huko ni kumfanyia Mungu dhihaka,” alisema Shehe Salum na kuongeza:
“Unajua suala la imani ni kitu kinachomhusu mtu binafsi, ni vyema kufanya uamuzi wa hakika na kushika njia moja na siyo kufanya dhihaka na dini ya Mwenyezi Mungu. Ni kitu kibaya sana.”
Naye Juma Suleiman, mkazi wa Ilala, jijini Dar es Salaam alimwambia mwandishi wetu kuwa, katika imani ya kiislam kunakatazwa watu kucheza na dini huku akisisitiza anayefanya hivyo anaweza kulaaniwa.
“Dini siyo kitu cha kuchezea, ni daraja la kumfikisha mtu kwenye haki, si mahala pa kuingia na kutoka, kuingia na kutoka. Huko ni kucheza na Mungu. Namshauri huyo mtoto (akimaanisha Wolper) abadilike. Asifanye mchezo na imani, Mungu anaweza kumlaani kwa kumchezea,” alisema Suleiman.

TUMEAMIA HUKU