Featured Posts

Friday, June 27, 2014

SOMA HII, MKE WA TYSON ATAKA MALI ZAKE, AMUHOFIA MONALISA

Wakati hata siku arobaini hazijatimia, mke wa marehemu George Otieno ‘Tyson’, Beatrice Shayo juzi alicharukia mali zake baada ya kuamua kutinga nyumbani kwa marehemu, Mbezi Makonde jijini Dar kwa lengo la kuchukua kila kinachomhusu. 

Mke wa marehemu George Otieno ‘Tyson’, Beatrice Shayo.
 Mdada huyo aliyefunga ndoa na Tyson Agosti 9, 2012 nchini Kenya na kujaaliwa kupata mtoto mmoja wa kiume aitwaye Eugene, alishuhudiwa na gazeti hili Juni 24, mwaka huu saa sita usiku akiwa na ndugu zake na kuanza kugonga geti la nyumba hiyo.
 Katika kujua kilichokuwa kikiendelea, mmoja wa mapaparazi wetu aliwasogelea na kuzungumza na Beatrice ambaye alieleza kuwa, lengo lake lilikuwa ni kuchukua mali zake zilizomo mle ndani.
“Ulidhani mimi nataka kuingia kwenye nyumba hii nikae, la hasha! Nimefuata mali zangu tu basi,” alisema Beatrice huku akiendelea kugonga geti hilo.


Mke wa Tyson (kulia) na ndugu zake wakisubili getini.
 Wakati Beatrice na nduguze wakionekana kukata tamaa ya kufunguliwa, mara alitokea mwanamke anayedaiwa alikuwa akiishi na marehemu mpaka kifo kilipomkuta na kuuliza aliyegonga geti ni nani, alipotajiwa jina la Beatrice alisema: “Eee, Beatrice, usiku huu umekuja kutafuta nini?”
Beatrice: Nina shida, naomba ufungue tuongee.

 Mwanamke: Hatuwezi kuongea usiku huu, uje kesho asubuhi.
Beatrice: Nakuomba ufungue tu, nimekuja kuchukua mali zangu nilizoacha humo ndani na nimekuja na gari kabisa la kubebea.

 Mwanamke: Mali gani, humu hamna chako na kama una kitu chako humu, fuata taratibu.
Beatrice: Nimefuata taratibu, nipo na mjumbe hapa.


George Otieno ‘Tyson’,enzi za uhai wake.
 Mwanamke: Ndiyo nasema mje kesho asubuhi na mapema mtanikuta.
Baada ya mwanamke huyo kugoma kufungua, mjumbe wa eneo hilo aliyefahamika kwa jina la Sabina Mawanda aliwashauri waondoke na kurudi tena asubuhi lakini inadaiwa walipofanya hivyo walikuta nyumba imefungwa na hakukuwa na mtu.

TUMEAMIA HUKU