Featured Posts

Monday, June 30, 2014

BABY MADAHA: SIOLEWI KWA KUFUATA MKUMBO


‘Baby Madaha’ akiwa kwenye pozi.

STAA wa muziki na filamu Bongo, Baby Joseph Madaha ‘Baby Madaha’ amesema anaishi katika staili ya kivyake hivyo kamwe hawezi kuolewa kwa kufuata mkumbo kama ilivyo kwa wasanii wengine. 
Staa wa muziki na filamu Bongo, Baby Joseph Madaha ‘Baby Madaha’
Akipiga stori na paparazi, Baby Madaha alikiri kuwa ana mchumba ambaye ni Joh Kairuki, anampenda sana ila katika suala la kufunga ndoa bado yupoyupo sana kwa sababu haolewi kwa kufuata mkumbo kwani amejifunza kupitia kwa walioolewa na kuachika.
“Nitaolewa nitakapokuwa tayari siyo kwa kufuata mkumbo vinginevyo bora nibakie hivihivi kwa sababu pesa kwangu ndiyo kila kitu, mambo mengine yanafuata,” alisema.

TUMEAMIA HUKU