Featured Posts

Monday, June 30, 2014

MAJANGA, MTOTO MIAKA 6, HAKUI, HAONGEI TAFADHALI SOMA HAPA UMSAIDIE MTOTO HUYU

HUSSEIN Jumbe ni mtoto mwenye miaka 6 sasa, lakini hakui, kwani hajaweza kukaa  wala  kuongea, mwonekano wake ni sawa na mtoto wa  mwaka mmoja, imekuwa kilio  na majonzi kwa mama yake  mzazi, Rukia Twalibu, mkazi wa Kilwa –Masoko, Mkoa wa Lindi.
Mtoto Hussein Jumbe  mwenye umri wa miaka 6 sasa.
Akizungumza kwa masikitiko makubwa na Uwazi mwishoni mwa wiki iliyopita katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Rukia alisema alimzaa  Hussein mwaka 2008 huko Kilwa lakini katika kukua  imekuwa ni tatizo kubwa  ambalo linaambatana na kushindwa kuongea wala kukaa.
“Hapa unapomuona anasikia kila kitu, anajua kila unachomuuliza lakini  hawezi kukaa wala kuongea. Muda mrefu nampakata au  analala tu,” alisema mwanamke huyo.
Mtoto Hussein Jumbe akiwa na mama yake mzazi, Rukia Twalibu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH).
Alisema baada ya mwanaye huyo kufikisha miaka miwili, baba yake mzazi alitoweka katika mazingira  ya kutatanisha hadi sasa  hajulikani alipo kitu ambacho  kimempa wakati mgumu sana.
Akaendelea: “Nilipobaini hali hii ya mtoto na sina msaada, nilikwenda Hospitali ya CCBRT (jijini Dar) lakini madaktari wa hospitali hiyo walisema ukubwa wa tatizo la mwanangu  hawawezi kufanya chochote.
“Juni 22, mwaka huu ndiyo nilikuja hapa Muhimbili ambapo  mwanangu anachunguzwa kisa cha kutokua kama watoto wengine ilhali umri unakwenda, bado madaktari hawajaniambia chochote, naamini wanaumiza kichwa kujua tatizo.
Bi. Rukia akijaribu kumkalisha mwanaye.
“Hadi kufika hapa Muhimbili nimepata michango kwa watu  pia nilipata barua kutoka Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Masasi  ambayo ilinisaidia kupata kiasi  kadhaa cha pesa,” alisema mama huyo.
Rukia na mwanaye amelazwa  katika Wodi ‘A’ ya Watoto, kwa  aliyeguswa na tatizo la mtoto  Hussein, awasiliane na mama  yake kwa namba 0714 177 071.
Naamini ukimsaidia mtoto huyo, utapata baraka katika kila ukifanyacho.

TUMEAMIA HUKU