Featured Posts

Sunday, June 8, 2014

BONGO MOVIE SHAMSA FORD AZUNGUMZIA PICHA ZAKE ZINAZOMUONYESHA AKILA TUNDA NA MBUNGE

Picha hizo zinawaonyesha wawili hao wakiwa kitandani kwenye mahaba mazito. 

  
Shamsa Ford.
Shamsa ana umbo la kawaida ki-shape lakini msichana huyo anaonekana kuwa na umbo namba nane.

 
Jana baada ya kuona picha hizo ambazo zimesambaa  hasa kwenye kurasa za kisiasa kwenye mitandao ya kijamii zikimuandama mbunge huyo wa Chadema, mwandishi wetu alimtafuta Shamsa na kumueleza kila kitu na kwa kujiamini Shamsa alisema picha  hizo sio zake, zimetengenezwa na pia msichana anayeonekana kiumbo wako tofauti na hata sura na akasema anajiheshimu sana na ana familia yake asingeweza kufanya jambo kama hilo...
  
 Moja ya picha hizo tukiwa tumeikata kwa sababu za kimaadili

Alipoulizwa  kama anafahamiana na Mh. Salvatory Machemli pia alikana kujuana naye achilia mbali kuwahi kukutana naye.

 
"Zimedaiwa kuwa ni mimi but sio mimi, naomba uangalie hizo picha vizuri au kama upo WhatsApp nikutumie halafu uone je ni mimi, kabla sijakujibu" Alisema Shamsana  na  kuongeza;

"Si umbo tu,  hata sura ni tofauti, sijawahi hata kumuona huyo mheshimiwa, nahisi ni watu ambao wananichukia wanataka kunichafua, kiukweli nawaomba mashabiki wangu kabla ya kuanza kunihukumu waziangalie kwanza hizo picha vizuri, mimi nina familia na najiheshimu".

  
Kwa upande mwingine baadhi ya wachangiaji mitandaoni wamedai kuwa picha hizo ni za kutengenezwa kwa sababu Mh.Machemli ana kitambi lakini katika picha hizo hazimuonyeshi akiwa na kitambi, wengine wamesema kuwa picha hizo zimechukuliwa katika mtandao mmoja wa ng9no na kufanyiwa photoshop lengo lake likiwa ni kumchafua kisiasa mbunge huyo ambaye anadaiwa kukumbwa na misukosuko ya mara kwa mara.

TUMEAMIA HUKU