Featured Posts

Wednesday, September 17, 2014

KULIKONI, UNAAMBIWA IRENE UWOYA AAMUA KUTIMUKIA USWIZI,

 
Irene Uwoya.

TAARIFA zilizotua kwenye meza ya Bongowood zinadai kuwa, Irene Uwoya amekimbilia nchini Uswisi ambako amekwenda kucheki mchongo wa kucheza muvi akitokea pande za Msumbiji alikokwenda akiongozana na mwigizaji Juma Chikoka baada ya kupata shavu la kutengeneza matangazo ya biashara.
Baada ya kunyaka mchongo huo, Bongowood ilimsaka Chikoka ambaye alikiri Uwoya kutimkia Uswisi kwa dili la kucheza filamu.

TUMEAMIA HUKU