Featured Posts

Tuesday, September 23, 2014

MAUAJI YA KINYAMA, KIJANA AUAWA KWA KUCHOMWA CHOMWA VISU MARA ZAIDI YA TANO KIFUANI

 Tukio hili limetokea eneo la Bonanza kata ya Chamwino, Dodoma mjini. Kwa shuhuda wetu aliyekuwa eneo la tukio  amesema kuwa dereva wa bodaboda amekutwa amefariki  baada ya kuuliwa na watu wasiojulikana  na kisha watu hao kutoweka  bodaboda aliyokuwa akiendesha marehemu huyo.

 Hiki ni mojawapo ya kisu kinachosadikiwaa kutumika katika kufanya mauaji hayo ya dereva wa Bodaboda na kisha watu hao kutoweka na pikipiki. 
 
Dereva huyo wa bodaboda  amechomwa kisu maeneo ya tumboni na shingoni katika mwili wake na katika eneo la tukio kumekutwa visu viwili amavyo vinasadikika kutumiwa katika uharifu huo kando kidogo ya barabara na sehemu ulipokuwa mwili wa marehemu.(Picha na Alex wa Pamoja Blog)

 Damu ikiwa imetapakaa eneo la tukio
 Hii ni mojawapo ya sehemu aliyochomwa kisu dereva huyo wa bodaboda 
Baadhi ya mashuhuda wakiwa kwenye eneo la tukio

TUMEAMIA HUKU