Featured Posts

Wednesday, September 24, 2014

KUHUSU MSANII MADEE KUTIWA NGUVUNI KWA KOSA LA UKABAJI , HII HAPA PICHA KAMILI

Taarifa zimethibitishwa kuhusu staa wa hit single kama ‘pombe yangu’ ‘tema mate tuwachape’ na ‘ni shidaah’ Madee ambae ni msanii kutoka kundi la TipTop Connection kushikiliwa na Polisi. 
Kabla ya kuongea na meneja wa kundi hilo ambae ni Babtale, Gossip Cop Soudy Brown kwenye You heard inayosikika kupitia XXL ya CloudsFM J3-Ijumaa alisema ‘inasemekana Jumamosi iliyopita Madee aliporwa simu yake na watu wawili usiku huko Kigamboni’Babtale alipoulizwa akasema ‘Kwenye mida ya saa tisa usiku Madee wakati anatoka kwenye show Kigamboni kuna waporaji simu wakiwa kwenye pikipiki wakampora kwa hiyo ikabidi gari aliyokuwemo Madee ikiendeshwa na Kwebe ianze kuikimbiza ile pikipiki alafu wakaigonga pikipiki kwa nyuma, pikipiki ilivyodondoka yule aliekua nyuma kwenye pikipiki ambae ndio alipora simu akafanikiwa kukimbia hivyo wakaishia tu kumkamata aliekua anaendesha hiyo pikipiki’ 

‘Wakamchukua na kwenda nae maskani Tiptop… mama yake akaja akasema msipeleke Polisi mwekeni hapa mi nakwenda kuwachukulia vitu vyenu, Madee kwa sababu alikua anakwenda kwenye show Mwanza ikabidi aende zake…… saa nne asubuhi yule mama akaja na Polisi badala ya kuja na mwizi mwenzake akaja na Polisi kataka kuwaokota watoto wote ofisini kwangu pale Tiptop, walimchukua huyo Muhalifu kwenye Land rover mpaka Polisi Magomeni na kubadilisha kibao kwamba huyu mtuhumiwa alitekwa’

TUMEAMIA HUKU