Featured Posts

Wednesday, September 24, 2014

BAADA YA AROBAINI YA MAMA TUNDA, AFANDE SELE ANASWA LIVE USIKU AKIWA NA DEMU MPYA

MKONGWE wa muziki wa kizazi kipya Seleman Msindi ‘Afande Sele’, juzikati alinaswa akiwa na demu mpya akiwa ni siku moja tu baada ya kufanyika kwa 40 ya aliyekuwa mzazi mwenzake, marehemu mama Tunda.
Mkongwe wa muziki wa kizazi kipya Seleman Msindi ‘Afande Sele’,akiwa na mpenzi mpya.
Tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia Septemba 21 mwaka huu ndani ya Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro wakati staa huyo aliyekuwa mmoja wa watoa burudani katika tamasha la Fiesta, alipoonekana akiingia akiwa ameambatana na mrembo mmoja akiwa ameshikana naye kimahaba.
Akiwa ndani ya uwanja huo, mkali huyo wa mashairi yenye vina kwa muda mwingi alikuwa pamoja na msichana huyo ambaye hakufahamika jina, wakiwa na dalili zote za wapendanao.
Mkali wa 'Rhymes' Bongo, Seleman Msindi ‘Afande Sele.
Alipoulizwa juu ya suala hilo, Afande Sele alicheka na kumtaka paparazzi wetu kuachana na masuala hayo aliyoyaita binafsi, badala yake asubiri apande jukwaani apate picha za kazi atakayofanya.

TUMEAMIA HUKU