Featured Posts

Wednesday, May 28, 2014

MWANAUME FAHAM WANAWAKE WANAPENDA NINI KUTOKA KWA WANAUME

Kama mwanaume lazima upate wakati 
wa kujua unatakiwa kufanya nini kwa ajili 
ya kulifanya penzi lako lizidi kuchanua. 
USAFI BINAFSI 
Asilimia kubwa ya wanawake wanapenda 
sana usafi. Ni aghalabu sana kukutana na 
mwanamke asiyejipenda. Ndiyo maana 
wanaitwa mapambo ya nyumba au la 
nyumba! Ni kwa sababu ya hulka yao ya 
kupenda sana usafi. 
Mwanamke anavutiwa sana na mwanaume 
mtanashati. Usafi wako unamfanya ajiamini 
kuwa na wewe. Hata nyumbani kwako, 
lazima uishi katika nyumba safi. Hata 
anapokuja kukutembelea, anakuta 
mazingira masafi kuanzia sebuleni hadi 
chumbani. 
Anapokukuta katika hali ya usafi, inakuwa 
rahisi zaidi yeye kuanzia hapo alipokukuta 
na kuendelea mbele. 
KUJIAMINI 
Mwanamke anajisikia salama zaidi akiwa na 
mwanaume ambaye anajiamini – mwenye 
uwezo wa kutetea hoja zake na kujieleza 
sawia. Siyo anayebabaika. Suala la msimamo 
binafsi, kwa mwanamke ni kubwa kuliko 
hata kumnunulia manukato mapya! 
Mathalani unakuwa naye katika mtoko, 
angependa kukuona ukiwa katika hali halisi 
ya maisha yako, usiyeyumbishwa na 
mwenye kutoa maamuzi yasiyoyumba. 
Wakati mwingine, mwanamke anaweza 
kukupima hata katika jambo ambalo 
amekosea yeye, ataangalia unavyotoa 
maamuzi yako, lakini pia atafuatilia kuona 
kama utakuwa mwepesi wa kuyabadilisha. 
Anataka kuona msimamo wako muda wote. 
Mwenye kujiamini na mawazo yasiyo na 
matege wala makengeza! 
KUJITETEA 
Kipengele hiki hakina tofauti kubwa sana 
na kilichopita, lakini hapa ni kwenye 
upande wa kujitetea zaidi. Wakati unapodai 
haki yako mbele ya mwanamke wako, suala 
la kujitetea linapewa nafasi kubwa sana. 
Wanawake hawapendi kuwa na wanaume 
ambao wapo tayari kuonewa. Wanataka 
wenye uwezo wa kusimama kidete kuona 
haki zao hazichukuliwi kirahisi. 
Hili si suala la kutetea tu haki yako pekee 
kama mwanaume, bali inapobidi kusimamia 
haki ya mwanamke wako. Nisieleweke 
vibaya katika hili, lakini mwanaume imara ni 
yule ambaye ana nguvu – anafanya mazoezi 
na ambaye yupo tayari kwa lolote! 
Inapowezekana, uwe na uwezo wa 
'kuzichapa' ikiwa mtakutana na vibaka au 
watu wabaya wenye lengo wa kukudhuru/ 
kuwadhuru au kumdhuru mpenzi wako. 
Mwanaume aliye 'fiti' ni chaguo la 
wanawake wengi. Si mnyonge. Mpole 
kupitiliza na aliye tayari kuonewa! Huyu 
hana nafasi. 
KUJALI 
Wanawake wanapenda sana wanaume 
wanaojali. Wanawaona wao ni kila kitu na 
wanaotoa kipaumbele kwao. Kama huna 
tabia hiyo, ujue upo katika nafasi kubwa ya 
kumkwaza mpenzi wako. Mjali mpenzi 
wako kwa kila hali. 
Kumjulia hali kila wakati na kutaka kujua 
maendeleo yake, kutakupa nafasi kubwa 
sana ya kuendelea kudumu katika uhusiano 
hai. 
UKARIBU 
Kati ya vitu vinavyowapa mshawasha 
mkubwa wanawake ni pamoja na 
kusogezwa karibu. Hapa ni kuwa naye 
katika mambo mengi unayoyafanya kila 
siku. 
Ni vizuri kuwasiliana naye mchana, ukitaka 
kujua aina ya chakula alichokula siku hiyo 
au ikiwezekana mchagulie. Ni mambo 
madogo sana lakini yanayoongeza nakshi 
katika mapenzi. 
Yapo mengi sana ambayo kwa kuyafanya 
utakuwa umemsogeza mpenzi wako karibu 
yako. Hebu tumia ubunifu wako ili uweze 
kuteka hisia za mwenzi wako kisawasawa! 
KUMSIFIA 
Wanaume wengi hupuuzia hili, huona kama 
ni jambo lisilo na maana sana kwao na 
wenzi wao. Hali ni tofauti sana kwa 
wanawake ambao hupenda kuwasifia 
wanaume zao. Nitakupa mifano miwili ya 
namna wanandoa wa jinsia mbili tofauti 
wanavyotambulishana kwa jamaa zao. 
MWANAUME: "Peter kutana na mke wangu, 
anaitwa mama Diana. Nipo naye mwaka wa 
tatu sasa, tuna watoto wawili, huyo Diana 
na mwingine anaitwa Cris. Mama Diana, 
huyu ni Peter nilisoma naye A – Level, 
Tosamaganga Sekondari." 
MWANAMKE: "Suzan, huyu ndiye mume 
wangu mpenzi...anaitwa Elifaraja lakini 
mimi napenda zaidi kumuita Elly. Kiukweli 
nampenda sana mume wangu jamani, tuna 
mtoto wetu mmoja, anaitwa Agness. 
(Akimgeukia mumewe) Baby, huyu hapa ni 
rafiki yangu Suzan. Yaani tumekua naye 
mtaa mmoja huko Arusha." 
ANGALIA TOFAUTI 
Bila shaka kwa namna wawili hao 
walivyotambulishana unaweza kuona 
tofauti kubwa. Mwanaume 
amemtambulisha mkewe kawaida kabisa, 
hajaonesha manjonjo au namna 
anavyompenda na kumthamini mwenzake, 
lakini mwanamke amefanya hivyo. 
Sikia nikuambie, KUMSIFIA mwanamke, 
kuna nafasi kubwa sana kwake. Chunguza 
kwa makini, hata kunapokuwa na 
mgongano katika familia, halafu wakatokea 
wageni, baada ya utambulisho na 
mazungumzo ya hapa na pale, wageni 
wakiondoka kunakuwa na uwezekano 
mkubwa zaidi wa kumaliza mpasuko katika 
familia. 
Jenga utamaduni wa kumsifia mpenzi 
wako, unamuweka katika kilele cha 
upendo. Anajiona kamili, peke yake na 
mwenye nguvu kwako. Anajiamini na 
unamfanya azidi kukupenda kwa kuwa 
anaamini yupo na mwanaume ambaye 
anajivunia kuwa naye. 
MALENGO 
Wanaume wengi wana ulemavu mmoja; 
hawapendi kuwashirikisha wanawake 
katika mambo yao. Wanapenda kufanya 
mambo yao kwa siri na wakati mwingine 
ikilazimika kumwambia mkewe basi kwa 
mshtukizo baada ya kukamilisha jambo 
husika. 
Hii si sahihi. Dunia ya leo imebadilika rafiki 
zangu. Inawezekana wazee wa zamani 
walikuwa sahihi, maana ilikuwa ni suala la 
kununua ng'ombe na kuwaweka katika zizi 
kwenye kijiji cha jirani, halafu wanapewa 
malisho mazuri, baada ya miaka miwili 
wanazaliana, hapo ndipo anamweleza 
mkewe. 
Siku hizi dunia imebadilika, kuna mambo 
mengi. Kuna suala la hasara katika biashara, 
utapeli n.k. Mkeo ndiye rafiki yako mkubwa 
kuliko wote, ndiye ndugu yako wa karibu 
zaidi kuliko yeyote. Yes! Mkeo ndiye ndugu 
yako maana umetengeneza naye familia. 
Mmeshirikiana kuzaa watoto na kujenga 
maisha pamoja. 
Yeye anapaswa kujua mambo yako, ndiye 
mtetezi wako nambari wani. Mweleze juu 
ya malengo yako, wakati mwingine 
anaweza kukusaidia sehemu ambayo 
hukutarajia. 
Hata hivyo, kumshirikisha katika malengo 
yako, kunampa nguvu na nafasi ya kujiona 
mama katika familia yenu. Msaidizi kamili 
wa nyumba yenu. 
KIPAUMBELE 
Kuna wakati wanawake huwa na mambo 
yao binafsi. Kazini au kifamilia. 
Inawezekana akatatizika katika eneo fulani 
ambalo kwa namna moja ama nyingine 
atahitaji usaidizi wako. Ikitokea mkeo 
akawa katika hali hiyo, msikilize. 
Mathalani ana tatizo la kifamilia, 
amekuambia mmoja wa wazazi wake 
anaumwa, msaidie. Si lazima kifedha, lakini 
kuonesha kujali kwako tu, kutampa 
matumani kwamba anaishi na mtu sahihi. 
Acha kupuuza mambo yake; hata yale 
madogo, kama ya 'mtoto wa dada 
amerudishwa ada shuleni'. 
Msikilize, mshauri panapofaa kufanya hivyo 
na ukiweza msaidie hata kifedha. Katika 
upande wa pili ni hivyo hivyo. Labda una 
tatizo binafsi, kazini kwako au kifamilia, 
mshirikishe. 
Unaweza kushangaa jambo ambalo 
uliamini unaweza kulimaliza peke yako, kwa 
kumshirikisha likawa jepesi zaidi na 
mambo yakaendelea vyema. Kipaumbele 
kwa namna yoyote ile, kunaongeza 
mapenzi zaidi kwa mwanamke. 
TENDO LA NDOA 
Hiki ni kipengele nyeti, kinachohitaji lugha 
nzuri ya kirafiki kukifafanua. Hakuna 
siri, tendo la ndoa ni moja ya kiwakilishi 
cha ndoa. Maana hata maandiko yanasema: 
"Mwanamke ataacha wazazi wake na 
kwenda kwa mumewe, nao watakuwa 
mwili mmoja." 
Kimsingi tendo la ndoa lina nafasi yake. Ni 
muhimu likaheshimiwa na kutengewa 
muda maalum wa kufurahia. Si papara. Kwa 
bahati mbaya wanaume huwa si 
wafuatiliaji sana wa kujua namna ya 
kuwafurahisha zaidi wenzao. Wenyewe 
wanajiwazia wenyewe. Wanafikiria namna 
ya kuwakomoa wenzao. 
Si sahihi. 
Tendo la ndoa halina maana ya 
kukomoana. Jenga mazoea ya kufanya 
maandalizi kamili kabla ya tendo. Sikiliza 
hisia za mwenzako. Ukiweza kumjulia mke 
wako katika eneo hili, ni wazi kwamba 
utazidisha upendo wake kwako, lakini pia 
atakuwa katika kuta za uaminifu. Akatafute 
nini nje wakati wewe ndiye mganga wake 
unayeweza kumtibu barabara? 
Kuna kitu nimesahau kweli? Kama kipo 
nitafute pembeni, kwa hapa haya yatoshe 
kukufanya uelewe nilichotaka kukuelekeza. 
Nikuache na neno moja; uamuzi 
wa kuijenga ndoa yako upo mikononi 
mwako. Ukitaka iwe shaghalabaghala, pia 
ni wewe tu!
Kama mwanaume lazima upate wakati 
wa kujua unatakiwa kufanya nini kwa ajili 
ya kulifanya penzi lako lizidi kuchanua. 
USAFI BINAFSI 
Asilimia kubwa ya wanawake wanapenda 
sana usafi. Ni aghalabu sana kukutana na 
mwanamke asiyejipenda. Ndiyo maana 
wanaitwa mapambo ya nyumba au la 
nyumba! Ni kwa sababu ya hulka yao ya 
kupenda sana usafi. 
Mwanamke anavutiwa sana na mwanaume 
mtanashati. Usafi wako unamfanya ajiamini 
kuwa na wewe. Hata nyumbani kwako, 
lazima uishi katika nyumba safi. Hata 
anapokuja kukutembelea, anakuta 
mazingira masafi kuanzia sebuleni hadi 
chumbani. 
Anapokukuta katika hali ya usafi, inakuwa 
rahisi zaidi yeye kuanzia hapo alipokukuta 
na kuendelea mbele. 
KUJIAMINI 
Mwanamke anajisikia salama zaidi akiwa na 
mwanaume ambaye anajiamini – mwenye 
uwezo wa kutetea hoja zake na kujieleza 
sawia. Siyo anayebabaika. Suala la msimamo 
binafsi, kwa mwanamke ni kubwa kuliko 
hata kumnunulia manukato mapya! 
Mathalani unakuwa naye katika mtoko, 
angependa kukuona ukiwa katika hali halisi 
ya maisha yako, usiyeyumbishwa na 
mwenye kutoa maamuzi yasiyoyumba. 
Wakati mwingine, mwanamke anaweza 
kukupima hata katika jambo ambalo 
amekosea yeye, ataangalia unavyotoa 
maamuzi yako, lakini pia atafuatilia kuona 
kama utakuwa mwepesi wa kuyabadilisha. 
Anataka kuona msimamo wako muda wote. 
Mwenye kujiamini na mawazo yasiyo na 
matege wala makengeza! 
KUJITETEA 
Kipengele hiki hakina tofauti kubwa sana 
na kilichopita, lakini hapa ni kwenye 
upande wa kujitetea zaidi. Wakati unapodai 
haki yako mbele ya mwanamke wako, suala 
la kujitetea linapewa nafasi kubwa sana. 
Wanawake hawapendi kuwa na wanaume 
ambao wapo tayari kuonewa. Wanataka 
wenye uwezo wa kusimama kidete kuona 
haki zao hazichukuliwi kirahisi. 
Hili si suala la kutetea tu haki yako pekee 
kama mwanaume, bali inapobidi kusimamia 
haki ya mwanamke wako. Nisieleweke 
vibaya katika hili, lakini mwanaume imara ni 
yule ambaye ana nguvu – anafanya mazoezi 
na ambaye yupo tayari kwa lolote! 
Inapowezekana, uwe na uwezo wa 
'kuzichapa' ikiwa mtakutana na vibaka au 
watu wabaya wenye lengo wa kukudhuru/ 
kuwadhuru au kumdhuru mpenzi wako. 
Mwanaume aliye 'fiti' ni chaguo la 
wanawake wengi. Si mnyonge. Mpole 
kupitiliza na aliye tayari kuonewa! Huyu 
hana nafasi. 
KUJALI 
Wanawake wanapenda sana wanaume 
wanaojali. Wanawaona wao ni kila kitu na 
wanaotoa kipaumbele kwao. Kama huna 
tabia hiyo, ujue upo katika nafasi kubwa ya 
kumkwaza mpenzi wako. Mjali mpenzi 
wako kwa kila hali. 
Kumjulia hali kila wakati na kutaka kujua 
maendeleo yake, kutakupa nafasi kubwa 
sana ya kuendelea kudumu katika uhusiano 
hai. 
UKARIBU 
Kati ya vitu vinavyowapa mshawasha 
mkubwa wanawake ni pamoja na 
kusogezwa karibu. Hapa ni kuwa naye 
katika mambo mengi unayoyafanya kila 
siku. 
Ni vizuri kuwasiliana naye mchana, ukitaka 
kujua aina ya chakula alichokula siku hiyo 
au ikiwezekana mchagulie. Ni mambo 
madogo sana lakini yanayoongeza nakshi 
katika mapenzi. 
Yapo mengi sana ambayo kwa kuyafanya 
utakuwa umemsogeza mpenzi wako karibu 
yako. Hebu tumia ubunifu wako ili uweze 
kuteka hisia za mwenzi wako kisawasawa! 
KUMSIFIA 
Wanaume wengi hupuuzia hili, huona kama 
ni jambo lisilo na maana sana kwao na 
wenzi wao. Hali ni tofauti sana kwa 
wanawake ambao hupenda kuwasifia 
wanaume zao. Nitakupa mifano miwili ya 
namna wanandoa wa jinsia mbili tofauti 
wanavyotambulishana kwa jamaa zao. 
MWANAUME: "Peter kutana na mke wangu, 
anaitwa mama Diana. Nipo naye mwaka wa 
tatu sasa, tuna watoto wawili, huyo Diana 
na mwingine anaitwa Cris. Mama Diana, 
huyu ni Peter nilisoma naye A – Level, 
Tosamaganga Sekondari." 
MWANAMKE: "Suzan, huyu ndiye mume 
wangu mpenzi...anaitwa Elifaraja lakini 
mimi napenda zaidi kumuita Elly. Kiukweli 
nampenda sana mume wangu jamani, tuna 
mtoto wetu mmoja, anaitwa Agness. 
(Akimgeukia mumewe) Baby, huyu hapa ni 
rafiki yangu Suzan. Yaani tumekua naye 
mtaa mmoja huko Arusha." 
ANGALIA TOFAUTI 
Bila shaka kwa namna wawili hao 
walivyotambulishana unaweza kuona 
tofauti kubwa. Mwanaume 
amemtambulisha mkewe kawaida kabisa, 
hajaonesha manjonjo au namna 
anavyompenda na kumthamini mwenzake, 
lakini mwanamke amefanya hivyo. 
Sikia nikuambie, KUMSIFIA mwanamke, 
kuna nafasi kubwa sana kwake. Chunguza 
kwa makini, hata kunapokuwa na 
mgongano katika familia, halafu wakatokea 
wageni, baada ya utambulisho na 
mazungumzo ya hapa na pale, wageni 
wakiondoka kunakuwa na uwezekano 
mkubwa zaidi wa kumaliza mpasuko katika 
familia. 
Jenga utamaduni wa kumsifia mpenzi 
wako, unamuweka katika kilele cha 
upendo. Anajiona kamili, peke yake na 
mwenye nguvu kwako. Anajiamini na 
unamfanya azidi kukupenda kwa kuwa 
anaamini yupo na mwanaume ambaye 
anajivunia kuwa naye. 
MALENGO 
Wanaume wengi wana ulemavu mmoja; 
hawapendi kuwashirikisha wanawake 
katika mambo yao. Wanapenda kufanya 
mambo yao kwa siri na wakati mwingine 
ikilazimika kumwambia mkewe basi kwa 
mshtukizo baada ya kukamilisha jambo 
husika. 
Hii si sahihi. Dunia ya leo imebadilika rafiki 
zangu. Inawezekana wazee wa zamani 
walikuwa sahihi, maana ilikuwa ni suala la 
kununua ng'ombe na kuwaweka katika zizi 
kwenye kijiji cha jirani, halafu wanapewa 
malisho mazuri, baada ya miaka miwili 
wanazaliana, hapo ndipo anamweleza 
mkewe. 
Siku hizi dunia imebadilika, kuna mambo 
mengi. Kuna suala la hasara katika biashara, 
utapeli n.k. Mkeo ndiye rafiki yako mkubwa 
kuliko wote, ndiye ndugu yako wa karibu 
zaidi kuliko yeyote. Yes! Mkeo ndiye ndugu 
yako maana umetengeneza naye familia. 
Mmeshirikiana kuzaa watoto na kujenga 
maisha pamoja. 
Yeye anapaswa kujua mambo yako, ndiye 
mtetezi wako nambari wani. Mweleze juu 
ya malengo yako, wakati mwingine 
anaweza kukusaidia sehemu ambayo 
hukutarajia. 
Hata hivyo, kumshirikisha katika malengo 
yako, kunampa nguvu na nafasi ya kujiona 
mama katika familia yenu. Msaidizi kamili 
wa nyumba yenu. 
KIPAUMBELE 
Kuna wakati wanawake huwa na mambo 
yao binafsi. Kazini au kifamilia. 
Inawezekana akatatizika katika eneo fulani 
ambalo kwa namna moja ama nyingine 
atahitaji usaidizi wako. Ikitokea mkeo 
akawa katika hali hiyo, msikilize. 
Mathalani ana tatizo la kifamilia, 
amekuambia mmoja wa wazazi wake 
anaumwa, msaidie. Si lazima kifedha, lakini 
kuonesha kujali kwako tu, kutampa 
matumani kwamba anaishi na mtu sahihi. 
Acha kupuuza mambo yake; hata yale 
madogo, kama ya 'mtoto wa dada 
amerudishwa ada shuleni'. 
Msikilize, mshauri panapofaa kufanya hivyo 
na ukiweza msaidie hata kifedha. Katika 
upande wa pili ni hivyo hivyo. Labda una 
tatizo binafsi, kazini kwako au kifamilia, 
mshirikishe. 
Unaweza kushangaa jambo ambalo 
uliamini unaweza kulimaliza peke yako, kwa 
kumshirikisha likawa jepesi zaidi na 
mambo yakaendelea vyema. Kipaumbele 
kwa namna yoyote ile, kunaongeza 
mapenzi zaidi kwa mwanamke. 
TENDO LA NDOA 
Hiki ni kipengele nyeti, kinachohitaji lugha 
nzuri ya kirafiki kukifafanua. Hakuna 
siri, tendo la ndoa ni moja ya kiwakilishi 
cha ndoa. Maana hata maandiko yanasema: 
"Mwanamke ataacha wazazi wake na 
kwenda kwa mumewe, nao watakuwa 
mwili mmoja." 
Kimsingi tendo la ndoa lina nafasi yake. Ni 
muhimu likaheshimiwa na kutengewa 
muda maalum wa kufurahia. Si papara. Kwa 
bahati mbaya wanaume huwa si 
wafuatiliaji sana wa kujua namna ya 
kuwafurahisha zaidi wenzao. Wenyewe 
wanajiwazia wenyewe. Wanafikiria namna 
ya kuwakomoa wenzao. 
Si sahihi. 
Tendo la ndoa halina maana ya 
kukomoana. Jenga mazoea ya kufanya 
maandalizi kamili kabla ya tendo. Sikiliza 
hisia za mwenzako. Ukiweza kumjulia mke 
wako katika eneo hili, ni wazi kwamba 
utazidisha upendo wake kwako, lakini pia 
atakuwa katika kuta za uaminifu. Akatafute 
nini nje wakati wewe ndiye mganga wake 
unayeweza kumtibu barabara? 
Kuna kitu nimesahau kweli? Kama kipo 
nitafute pembeni, kwa hapa haya yatoshe 
kukufanya uelewe nilichotaka kukuelekeza. 
Nikuache na neno moja; uamuzi 
wa kuijenga ndoa yako upo mikononi 
mwako. Ukitaka iwe shaghalabaghala, pia 
ni wewe tu!

TUMEAMIA HUKU