Featured Posts

Wednesday, May 28, 2014

JACK CHUZI AZUA GUMZO KWA WATU, NI BAADA YA KUFUMWA HOSPITALI AKIWA NA NJEMBA


MWIGIZAJI Jacqueline Pentezel ‘Jack wa Chuz’ akutwa na njemba aliyejulikana kwa jina la Rashid Said.
Baadhi ya watu waliofika kumtembelea Jack aliyekuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa Typhoid, walihoji juu ya ukaribu wa Rashid ambaye ni kinyozi mjini hapa na staa huyo ndipo paparazi wetu alipowauliza wawili hao kwa nyakati tofauti, kila mmoja akatoa jibu lake.
“Huyu ni shemeji yangu kwa bwana angu ambaye baada ya kupata taarifa za mimi kulazwa alifika hapa toka mwanzo na kunihudumia,” alisema Jack huku Rashid akisema:
“Jack ni rafiki yangu na kwamba baada ya mimi kupata taarifa za kuugua kwake, nilikuja kumhudumia.”
Jack baada ya kulazwa kwa muda hospitalini hapo, aliruhusiwa na kurejea nyumbani kwake, Dar.

TUMEAMIA HUKU