STAA wa vichekesho, Sherry Magali ambaye pia ni mtoto wa msanii wa filamu Charles Magali amepata ajali na kuvunjika mguu alipokuwa njiani akielekea kwenye msiba wa George Otieno ‘Tyson’.
Chanzo kilichoshuhudia ajali hiyo kilieleza kuwa, ilitokea maeneo ya Sinza Kijiweni jijini Dar akiwa amepakizwa kwenye pikipiki gari ndogo iliwagonga kwa nyuma na kumfanya avunjike mguu.
Katika kujua ukweli wa tukio hilo,Sherry ambaye alisema:
Katika kujua ukweli wa tukio hilo,Sherry ambaye alisema:
“Ilkuwa ajali mbaya sana, niliona roho yangu inaondoka hivihivi. Dereva hakuumia sana ila mimi niliumia na kupelekwa pale Hospitali ya Palestina, nilipopigwa X-Ray ikabainika mguu umevunjika wakanifunga hogo.”