Featured Posts

Friday, May 9, 2014

YANGA SASA KUMEKUCHA... WACHUKUA STREKA WA CAMEROON. ANAFUNGA MPAKA KWA KISIGINO

YANGA imepanga kumsainisha rasmi mkataba kiraka Mbuyu Twite mchana huuu lakini imetegesha rada zake Cameroon kupata straika la maana kuziba nafasi ya Didier Kavumbagu aliyechepukia Azam FC.
Akizungumza na Mwanaspoti Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Yanga,Mussa Katabaro alisema tayari wameshapokea ripoti ya kocha wa Hans Pluijm ambaye ametaka kusakwa kwa nguvu zote mshambuliaji mpya akiwa na sifa mbili kubwa.

Katabaro alisema wanataka straika mwenye uwezo katika kufunga kwa kutumia miguu pamoja na vichwa kitu ambacho kilikuwa kinapungua kwa Mrundi Kavumbagu.

Alisema katika mchakato huo tayari rada zao zipo Afrika Magharibi hususani Cameroon ambapo kuna jina moja limefika mezani kwao na kazi imeshaanza kulimulika.

"Tunataka kufanya usajili wenye akili, hatutaki kukurupuka katika hilo, tunakutana mwisho wa wiki hii kufuatilia mambo fulani ya wapi tutampata mtu muafaka atakayetusahaulisha Kavumbagu haraka na wapo wengi kwa mujibu wa kocha wetu (Pluijm)," alisema Katabaro.

"Tumeanza kazi hiyo taratibu sio kwamba hatujaanza kabisa, kuna nchi kama Senegal na Cameroon ambako tumehakikishiwa na tunajipanga, tupeni muda tuisuke Yanga,"alisisitiza. Yanga haijatoa orodha kamili ya wachezaji inaowapukutisha ingawa kamati ya usajili imeweka bayana kwamba hakutakuwa na majina mengi makubwa.


TUMEAMIA HUKU