Featured Posts

Friday, May 9, 2014

JAMANI JAMANI HAWA WASANII WA BONGO WAMEZIDI SASA... TAZAMA WANAVODENDEKA MCHANA KWEUPEEE BILA WASIWASI

Wasanii  wasioishiwa  vituko  Tanzania, Miss  Ruvuma  2005  Isabela  Mpanda  na  Luteni  Karama  wameonekana  katika  viwanja  mbalimbali  vya  burudani  wakipeana  mahaba  momoto   na  kudai kuwa wanawakomesha  waliotia   doa  mapenzi  yao  na  kusababisha  yasambaratike....

Isabela  na  Karama  ambao  waligombana  na  kutengana  kabisa  kwa  madai  kuwa  Karama  siyo  mwaminifu  katika  mapenzi yao  walifikia  hatua  mbaya  ya  kurushiana  matusi  lakini  sasa  hivi  wamerudiana  na  kuwaacha  midomo  wazi  waliokuwa  wakishabikia  ugomvi  wao.....

"Sina  la  kuongea  kabisa, nilikuwa  sina  raha  kabisa  maishani  mwangu, nilikuwa  natumiwa  meseji  za  ajabu  lakini  niliomba Mungu  hatimaye  Karama  amerudi  katika  himaya  hii, hapana  chezea  Bella"  Alisema  Isabella
Aliongeza  kwa  kusema  kuwa  yeye  kama  Bella  ameamua  kutulia  na  Karama  kwa  sababu  ameona  michepuko  siyo  dili  na  inaweza  kumharibia  maisha  yake  na  watoto....


Hata  hivyo  baadhi  ya  marafiki  wa  Bella  wamedai  kuwa  hivi  sasa  Karama  amefika  kwa  Bella  kwani  haendi  katika  mishemishe zake  za  kila  siku  kwa  madai  kwamba  anamtuliza  mpenzi  wake  aliyekuwa  na  ugomvi  naye

TUMEAMIA HUKU