Featured Posts

Tuesday, May 20, 2014

INASHANGAZA: KUAMBIANA AZUNGUKA KUAGA MASHABIKI BAA

KATIKA hali ya kushangaza, inaelezwa kuwa saa chache kabla ya kifo chake, staa wa filamu za Kibongo, marehemu Adam Kuambiana alipita katika baa mbalimbali za jijini Dar es Salaam kuaga mashabiki wake.

Jeneza lenye mwili wa Adam Kuambiana.
Habari kutoka kwa mtu wa karibu na Kuambiana zinasema kuwa, Ijumaa (siku moja kabla ya kifo chake) alionekana baa mbalimbali akizungumza na mashabiki wake, jambo lililoashiria kuwa ni kama alikuwa akiwaaga.
Adam Kuambiana.
“Alikwenda Shikamoo Pesa (Sinza Kwaremmy), Green Park (Mwenge), New Sinza (Kwa Remmy) Igo (Sinza Mori) ambapo alikaa hadi usiku wa manane. Alionekana mchangamfu sana na alizungumza na watu wengi sana siku hiyo. Ni kama alijua angekufa ndiyo maana akaamua kuagana na mashabiki wake,” alisema.

TUMEAMIA HUKU