Featured Posts

Sunday, July 6, 2014

YASEMEKANA ETI: WATAALAM WA MUZIKI WANASEMA, ENDAPO DIAMOND PLATNUMZ ASINGEFANYA HAYA BASI ASINGESHINDA TUZO HATA MOJA.


Ugomvi uliompelekea kubadili maisha yake.
Una habari kuwa kuna sababu zilizompelekea diamond kuzidi ku-make headlines siku hadi siku?, kama ilivyo kwa msanii yeyote yule mwenye mafanikio duniani, kuna ishu mbili tatu zilizowahi kumtokea katika maisha yake, ambazo ndio zilimpelekea kumsukuma, pamoja na jitihada za kujituma, kuweza kumfikisha hadi kwenye mafanikio yake. Kama ulikuwa hujui, basi bila Diamond kufanya haya, hii leo, hizo tuzo zote, kuanzia ya mtv na kili zingekuwa bado ni ndoto, na kwa hapa Tzee angekuwa na-hit tu kinyumbani nyumbani kama ilivyo kwa wasanii wengi wa bongo fleva.

10012448_682787231779836_1342742437_n

Rumors has it kwamba, bila Diamond kugombana na aliyekuwa manager wake wa zamani, hii leo asingekuwa amefikia hapa alipo, manyanyaso aliyoyapata hapo nyuma, akiwa na uongozi wake wa zamani, ndio iliyomsukuma kufanya vitu kwa bidii na kufikia hadi hii leo, mbali na struggle zake za kila siku katika kujitangaza kimuziki.

1diamond

Inasemekana kuwa management yake ya sasa ndio inayompa sapoti kubwa sana katika kufanya vitu ki-international zaidi, na jina lake kuzidi kukua ulimwenguni, hadi kwa hivi sasa watu wamesha msahau Diamond wa mbagala.


Alipoamua kufaya jambo la hatari katika muziki wake.

Cover

Kama ilivyo katika kila biashara, bila risk huwezi kupata kile ulichokuwa unatarajia, na wala huwezi kuendelea, utabaki hapo hapo siku zote, hii ndio mchezo aliofanya Dangote, kuanzia kutoka kufanya video za milioni mbili hadi kufikia mahali na kufanya video za zaidi ya milioni ishirini, kitendo hichi ndicho kilichopelekea Diamond Platnumz aweze kujulikana zaidi nchi mbali mbali, haswa kwa nyimbo yake ya “my Number1”. Ni moja kati ya vitu ambavyo matunda yake yanaonekana hadi leo, kwa kuendelea kukaa on top kwenye charts, hadi kumpelekea tuzo mbalimbali.

TUMEAMIA HUKU