Featured Posts

Wednesday, July 30, 2014

je wajua Wanawake Wanaoendesha Magari Wengi ni Viruka Njia, Hawatulii Nyumbani

Kuna malalamiko mengi yanatoka kwa wananume wenye wake au wapenzi wao ambao wanajua kuendesha magari kwamba wamekuwa kiguu na njia.

Jana nikiwa sehemu fulani, nikiwa na jamaa fulani tukawa tunapiga story mbili tatu hivi. Huyu jamaa akaniambia kuwa mke wake tangu ajue kuendesha gari mke wake hatulii nyumbani week end. Huwa anatafuta visingizio mbalimbali ili kuhalalisha safari zake hizo. huwa anasingizia anakwenda kitchen party, kupeleka watoto hospitali hata kama hawaumwi, au kwenye bithday mbalimbali hata kama anakokwenda hakuna undugu wa karibu au family friend. Siku za kazi wanaenda pamoja kazini na kurudi wote mara chache kwani mwanaume ana uwezo wa kutumia gari la kazini.

Nimeamua kulitoa hapa kwa sababu hata jirani alishanilalamikia kuhusu tabia za mke wake kuwa amekuwa kiguu na njia hasa wikiend wanapokuwa mapumziko kwa visingizio mbalimbali ambavyo vingine vinafanana na hivyo hapo juu.

Kwa upande wangu mimi nipo neutral, nawakarisha kama visa hivi ni vya kweli au uwongo. >

TUMEAMIA HUKU