Featured Posts

Thursday, July 31, 2014

BAADA YA MWEZI MTUKUFU, MASTAA WARUDI KWENYE VIVAZI VYAO VYA KUWAUMIZA WANAUME

Ndani ya mwezi mtukufu mastaa wengi walionekana kuvaa kiheshima huku wakijisitiri sehemu zao nyeti lakini cha ajabu mara baada ya mfungo, baadhi wamerejea mavazi yao ya kimitego.

Video queen Agnes Masogange akipozi.
Uchunguzi uliofanywa na Ijumaa mara baada ya Sikukuu ya Idd kupita umebaini baadhi wamerejea kwenye mavazi yao ya kihasara, mazingira yanayoashiria kuwa, walihamia kwenye mavazi ya kiheshima kinafiki.
Mrembo aliyeng’ara kwenye Shindano la Miss Tanzania mwaka 2011, Hamisa Hassan ‘Mabeto’.
Akizungumza na Ijumaa baada ya kumuona Wema Sepetu kwenye Uwanja wa Ndege wa Julias Nyerere akiwa amevaa taiti nyekundu iliyobana makalio yake, mdau mmoja aliyeomba hifadhi ya jina lake alisema:
Staa wa Filamu Bongo, Wema Sepetu akipozi na Ommy Dimpoz.
“Dah! Mwezi umeisha sasa tutakoma kwa mavazi ya kihasara, Wema alikuwa akijisiri sana ndani ya mwezi mtukufu lakini alivyovaa leo, daah.”

TUMEAMIA HUKU