Featured Posts

Sunday, September 21, 2014

WASTARA AFUNGUKA BILA KUPEPESA MACHO, UCHAFU WA BONGO MOVIE,

Stori: Mayasa Mariwata
Neno! Staa wa sinema za Kibongo, Wastara Juma, bila kumung’unya maneno amefunguka kwamba kufuatia mfarakano ndani ya Klabu ya Bongo Movie Unity hadi kufikia hatua ya aliyekuwa mwenyekiti wao, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ kujiuzulu, kumewachafua kwa viongozi serikalini hasa Rais Dk. Jakaya Mrisho Kikwete ‘JK’.
Staa wa sinema za Kibongo, Wastara Juma.
Akizungumza na Ijumaa Wikienda,  wikiendi iliyopita jijini Dar, Wastara alisema anawashangaa wasanii wenzake wanaoendekeza majungu kutokana na wivu wa maendeleo na kusababisha klabu hiyo kutosonga mbele badala na kuonekana kituko.
Wastara alisema kuwa jambo hilo lisiporekebishika hali haitakuwa shwari klabuni hapo hata kama atachaguliwa mwenyekiti mwingine.
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Bongo Muvi, Steve Nyerere akizungumza jambo.
“Kuna wakati inabidi wasanii tuambiane ukweli ili mambo yaende sawa,” alisema Wastara akisitiza mshikamano miongoni mwao.

TUMEAMIA HUKU