Kilichomkuta Farzana Parveen mwenye umri wa miaka 25 kinawakumba Wanawake wengi nchini Pakistan na katika nchi nyingine ambapo April 2014 Tume ya haki za binadamu nchini Pakistan ilisema Wanawake 869 nchini humo waliuwawa kwa namna hii nchini Pakistan.
Kikubwa kingine kilichohuzunisha ni kwamba Mwanamke huyu aliuwawa mbele ya Mahakama ambapo Baba mzazi wa Mwanamke huyu alijisalimisha Polisi baada ya kuhusika kwenye mauaji na kisha akasema hajutii kufanya hivyo kwa sababu ni aibu kubwa iliyoletwa kwenye familia na Marehemu.