Featured Posts

Monday, August 25, 2014

Sitaki Kusikia Tena Habari za Mtunisi Mimi na Yeye Mapenzi Yalikwisha

Stori: Gladness Mallya
WAMEMALIZANA! YOBNESH Yusuph ‘Batuli’ anayekimbiza kunako soko la Bongo Movies, amefunguka kuwa hataki kusikia habari za aliyekuwa mpenzi wake aliye pia msanii mwenzake, Mtunisi kwani mapenzi yalishaisha.

Akistorisha na paparazi wetu, Batuli alisema hataki kumsikia wala kujua habari za Mtunisi kwani mapenzi yalikuwa zamani lakini kwa sasa kila mtu ana maisha yake yaani yeye Mtunisi ana mke na yeye ana mpenzi wake.


“Mimi kwa sasa nina maisha yangu na Mtunisi ana maisha yake nawashangaa wanaoniandama kwa maneno kwamba bado niko naye, jamani Mtunisi ana mke na mimi nina mpenzi hivyo sitaki kusikia habari hizo  kabisa,” alisema Batuli.

TUMEAMIA HUKU