Featured Posts

Saturday, June 7, 2014

RAY C ADAI KUGOMBEA UBUNGE 2015 ILI KUPIGANA NA WATU WANAOINGIZA MADAWA YA KULEVYA NCHINI



Makundi  mengi  ya  vijana  ndani  ya  mtandao  wa  facebook  yamekuwa  na  imani  kuwa  msanii  Rehema  Chamila  anaweza  kuwa  mtetezi  wao  mkubwa  endapo  ataamua  kuingia  kwenye  siasa...

Vijana  hao  wanaamini  kuwa  Ray C kwa  sasa  amepitia  changamoto  nyingi   hivyo  wanaamini  kama  akipewa  nafasi  ya  kuingia  bungeni  inaweza  kuwa  chachu  ya yeye  kupigana  na  watu  wanaoingiza  madawa  ya  kulevya  nchini  na  kuwaokoa  vijana  wengi  wanaopotea  kutokana  na  matumizi  ya  dawa  hizo

"Ray C kwa  nini  asiingie  tu  kwenye  siasa  na  akatutetea  kwenye  mambo  ambayo  hata  yeye  alikutana  nayo  hadi  yakataka  kumtoa  roho, tunaamini  anaweza  endapo  ataamua  kufanya  hivyo" alidai  kijana  mmoja  ndani  ya  mtandao  wa  facebook

TUMEAMIA HUKU